Tuesday, September 20, 2011

UMUHIMU WA MARAFIKI

Katika jamii yeyote wa wanadamu ambao wana ishi pamoja na kushirikiana,marafiki ni watu ambao wana kuwepo.Hawa wanakuwa watu wa karibu na mtu fulani kwa shida na raha.Tunategemea kuona marafiki wakiwa wana furaha na amani pia waki shirikiana katika masuala mbalimbali katika maisha.

Yapo baadhi ya maswali ya kujiuliza mtu mwenyewe katika nafsi yako.Maswali hayo ni;Je urafiki nilionao na mtu fulani una faida au hasara? Lakini pia vema kujiuliza kama Urafiki huo katika maisha yako hauwezi kuwa na madhara.Madhara hayo yanaweza kuwa chanya au hasi.Hii ina maana kuwa ni vizuri kutambua umuhimu wa urafiki huo na athari zake.

Kwa sasa ulimwengu umekuwa katika matatizo mengi yanayotokana na urafiki.Matatizo haya yanaweza kuepukwa  kwa wanadamu kuwa waangalifu na watu ambao wana kuwa katika mahusiano ya urafiki.Uwe urafiki wa kawaida au wa kimapenzi.Hii itasaidia sana kujenga jamii ya marafiki walio bora na kuwa na urafiki mzuri na wenye mafanikio kwa pande zote husika.

Monday, June 27, 2011

KUMBE SHAGGY ALIPIGA SERENGETI????????














‘Shaggy’ alivyojiachia ndani ya Visiwa vya Zanzibar







Pichani ni mwanamuziki wa kimataifa wa ragga na mshindi wa tuzo za Grammy 2011, Orville Richard ‘Shaggy’ alivyojiachia ndani ya Visiwa vya Zanzibar wakati alipokuwa akielekea wa ajili ya tamasha la filamu za nchi za majahazi maalufu kama (Zanzibar International Film Festival-ZIFF) lililofanyika ndani ya Ngome kongwe na kufurika mamia wa mashabiki kumshuhudia mjamaika huyo anayeishi marekani.

SHAGGY ATAWAZWA KUWA CHIFU NA BALOZI WA KABILA LA WASUKUMA BUJORA, MWANZA

SHAGGY AKIWASILI MJINI MWANZA
 


 
Mwanamuziki Shaggy wa Marekani akiondoka kwa kucheza huku akiwa ameshikilia usinga na kusindikizwa na vigoli wa kabila la kisukuma wakati alipokuwa akiondoka katika eneo la tukio mara baada ya kutawazwa kuwa chifu wa kabila la wasukuma, katika tamasha la ngoma za asili la Siku ya Mavuno yaani (Bulabo) kwa Kisukuma lililofanyika katika kijiji cha Kisesa mahali ambapo pana makumbusho ya Bujora yaliyohifadhi tamaduni zote za kabila la wasukuma.

Mwanamuziki Shaggy akishangilia mara baada ya kumtawazwa kuwa chifu wa kabila la wasukuma katika kijiji cha Kisesa.
 



HAYA NDO MAMBO YA USIKU WA KHANGA ZA KALE

Pichani ni wanamuziki wa wana Njenje Band-The kilimanjaro wakiwa wametinga Khanga za kale wakati wakifanya onesho pale Salender Bridge Club


Washiriki wengine wakifurahia usiku wa kale.


Dida nae hakuachwa nyuma kwenye usiku wa khanga za kale

Thursday, June 23, 2011

AFRICA MAGIC SWAHILI KUANZA KUONEKANA LIVE JULAI MOSI MWAKA HUU…!!!

Mkurugenzi Mtendaji wa COSOTA Yustus Mkinga akifafanua juu ya hakimiliki za kazi za wasanii nchini katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha AFRICA MAGIC SWAHILI zilizofanyika jijini Dar es Salaam.

Katikati ni Mkurugenzi wa Multichoice Tanzania Peter Fauel akifuatilia kwa makini uzinduzi wa AFRICAN MAGI SWAHILI uliyofanyika katika Hoteli ya MovenPick jijini Dar es Salaam. Kituo hicho kitaanza kuonyeshwa rasmi Julai 1 siku ya Ijumaa kuanzia saa 11 jioni kupitia Channel 127.

Mkurugenzi wa MNET Africa Biola Alabi akifungua rasmi Channel  ya filamu za Kiswahili itakayojulikana kama AFRICAN MAGIC SWAHILI itakayokuwa ikipatikana katika Channel 127 kuanzia saa 11 jioni mpaka saa 5 usiku katika sherehe za ufunguzi zilizofanyika kwenye Hoteli ya  MovenPick jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi.

Baadhi ya wafanyakazi wa Multichoice Tanzania wakishuhudia uzinduzi huo.

Mmoja wa watengezaji filamu za kibongo maarufu kwa jina Mtitu akitoa hoja katika uzinduzi wa kituo cha AFRICA MAGIC SWAHILI zilizofanyika jijini Dar es Salaam.

Msanii Mkongwe wa filamu nchini Natasha maarufu kama Mama Monalisa akiwashukuru MNET AFRICA kwa kutambua na kuendeleza kazi zao nchini na Afrika Mashariki katika uzinduzi wa Kituo cha AFRICA MAGIC SWAHILI jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wasanii wa filamu za kibongo waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa kituo cha AFRICA MAGIC SWAHILI iliyofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia uzinduzi huo.

Muigizaji na Mtengenezaji Filamu za kibongo Steven Kanumba hakuwa nyuma katika kuchangia hoja mbalimbali kwenye uzinduzi huo.

Wednesday, June 22, 2011

Zawadi Za Vodacom Miss Mwanza zatangazwa









Hatimaye Zawadi za washindi wa Vodacom Miss Mwanza 2011, zimetangazwa leo katika ukumbi wa Hoteli mpya ya Gold Crest iliyopo katikati ya jiji la Mwanza. Akitangaza zawadi hizo Katibu wa Sisi Entertainment Mukhsin Mambo maarufu Mc Stopper ameeleza, kifuta jasho kwa washiriki nafasi ya sita hadi ya kumi na nne watapata Tsh. 100,000/=

Nafasi ya Tano- 200,000/= Nafasi ya Nne- 200,000/= nafasi ya Tatu- 300,000/= Nafasi ya Pili- 500,000/= na Vodacom Miss Mwanza 2011- 1,000,000/=

Hii ni kwa mara ya kwanza kwa Miss Mwanza kuzawadiwa donge nono la Tshs. 1,000,000/=


Warembo hao pia walipata fursa ya kutembelea ofisi za Vodacom Mwanza kushuhudia shughuli zinazofanywa katika ofisi hizo.

Askofu Wa TAG Aiponda Bajeti Ya Serikali, Asema Haina Lengo La Kumkomboa Masikini

HUKU wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania hasa wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) wakiipinga mapendekezo ya bajeti ya serikali kwwa mwaka wa fedha 2011/2012 iliyowasilishwa bungeni na waziri wa fedha na uchumi Mustafa Mkulo ,askafu wa kanisa la Tanzania Assembulise Of God (TAG) jimbo la Iringa Jonas Mkane (pichani) ameipinga bajeti hiyo kuwa haijalenga kumkomboa mwananchi wa kawaida.

Pamoja na kuipinga bajeti hiyo pia askofu huyo aliitaka serikali kuwashughulikia vikali mafisadi ambao ndio wanafanya watanzania kuishi maisha magumu.

Katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kufungua semina ya wachungaji wa jimbo la Iringa iliyofanyika TAG Mlandege ,askofu Mkane alisema kwa upande wake anaona kuwa bajeti hiyo haijalenga kumkomboa mwananchi wa kawaida .

Alisema kwa upande wake alifikiri kuwa kabla ya kutenga bajeti hiyo serikali inapaswa kushughulika na watu wachache ambao wamekuwa wakiichakaza nchi kwa kuendekeza ufisadi na baada ya hapo kukaa chini na kutenga bajeti ya wananchi itakayowatoa katika dimbwi laumaskini ila kuendelea kutenga bajeti hiyo na kuwakabidhi mafisadi ni kumkomoa mwananchi.

"Mimi nadhani kabla ya kutenga bajeti hiyo serikali inageanza kushughulika na watu wachache ambao wanafanya ufisadi ndani ya Taifa ambao wanafahamika soma zaidi